Welcome to MFA's Official Site....Its Amazing and Sports Oriented!
Friday, February 15, 2013
Ukata waitoa Vikindu Warriors ligi daraja 3 mkoa
Mmoja wa wadau wakubwa wa timu hiyo ambaye hakutaka kutaja jina lake alithibitisha kuwa tayari uongozi wa klabu hiyo umekiandikia chama cha mpira wa miguu mkoa wa Pwani [COREFA] kwa ajili ya kujiondoa katika ligi.
Timu hiyo ilishindwa kwenda mafia kucheza mechi zake mbili na klabu za Al-itihad na Wagadugu Fc mwishoni mwa mwezi uliopita.
Wadau wa soka wilayani hapa wameelezea kusikitishwa kwao na hali iliyojitokeza kutoka na wilaya hiyo kubakiwa na timu moja tu ya Black Tiger katika ligi hiyo inayoendelea kutokana na timu nyingine ya Binga Stars kushindwa kushiriki kwa sababu za ukosefu wa fedha kama ilivyo kwa vikindu.
Subscribe to:
Comments (Atom)
